WhatsApp Group Join Now

MAJINA ya Walioitwa Kwenye Usaili UTUMISHI June 2026

Filed in Usaili by on June 9, 2026 0 Comments
MAJINA ya Walioitwa Kwenye Usaili UTUMISHI

MAJINA ya Walioitwa Kwenye Usaili UTUMISHI

Utumishi inapenda kuwataarifu Waombaji Kazi wote walioomba kazi kuwa usaili unatarajiwa kuendeshwa hatimaye kuwapangia vituo vya kazi waombaji kazi watakaofaulu usaili huo. Wasailiwa wanaoitwa kwenye usaili wanapaswa kuzingatia maelekezo
yafuatayo:-
1. Usaili utafanyika kuanzia tarehe kama ilivyooneshwa kwenye tangazo hili muda na sehemu ambapo usaili utafanyika umeainishwa kwa kila Kada.
2. Kila msailiwa anatakiwa kufika kwenye eneo la usaili akiwa amevaa Barakoa (Mask).
3. Kila Msailiwa anapaswa kuwa na kitambulisho kwa ajili ya utambuzi. Vitambulisho vinavyokubalika ni pamoja na:- Kitambulisho cha Mkazi, Kitambulisho cha Mpiga kura, Kitambulisho cha kazi, Kitambulisho cha Uraia, Hati ya kusafiria, Leseni ya Udereva au barua ya
utambulisho kutoka Serikali ya Mtaa/Kijiji anachotoka.
4. Wasailiwa wanatakiwa kufika na VYETI VYAO HALISI, kuanzia cheti cha kuzaliwa, kidato cha IV, VI, Astashahada, Stashahada, Stashahada ya Juu, Shahada na kuendelea kutegemeana na sifa za nafasi husika.
5. Wasailiwa watakaowasilisha ‘Testimonials, Provisional Results, Statement of results’, hati za matokeo za kidato cha IV na VI (‘form IV and form VI results slips’) HAVITAKUBALIWA NA HAWATARUHUSIWA KUENDELEA NA USAILI.
6. Kwa kada ambazo wanatakiwa kusajiliwa na Bodi za Kitaaluma wanapaswa kuja na vyeti vyao Halisi vya Usajili pamoja na Leseni za kufanyia kazi.
7. Kila msailiwa atajigharamia kwa Chakula, Usafiri na Malazi. Aidha kila msailiwa anapaswa kuhudhuria usaili akiwa na mavazi nadhifu na yenye staha kulingana na Waraka wa mavazi.
8. Kwa wasailiwa waliosoma nje ya Tanzania wahakikishe Vyeti vyao vimehakikiwa na kuidhinishwa na Mamlaka husika (kama TCU, NACTVET au NECTA). Wasailiwa wa kada zinazohitaji ‘GPA’ waliosoma nje ya Tanzania wawasilishe cheti cha ukokotozi wa GPA kutoka TCU.
9. Wasailiwa ambao hawajaona majina yao kwenye tangazo hili wanapaswa kuingia kwenye akaunti zao za ‘Ajira Portal’ na kuona sababu za kutokuitwa kwao ili wasikose fursa wakati mwingine.
10. Wasailiwa wote walioitwa kwenye usaili wahakikishe wanaingia kwenye akaunti zao na kunakili namba ya usaili. Aidha wasailiwa watakaofanya usaili wa mchujo kwa njia ya Mtandao wanapaswa kukumbuka barua pepe (email address) na nywila (password) zao wanazotumia katika mfumo wa Ajira Portal.
11. Wasailiwa ambao majina yao yanatofautiana katika nyaraka zao wanapaswa kuwasilisha Hati ya Kiapo cha Kubadili Jina (Deed Poll) iliyosajiliwa na Wizara ya Ardhi.
12. Waombaji wote wa kazi wanakumbushwa kuwa ni marufuku kutoa au kupokea rushwa kwa lengo la kupata ajira au kupangiwa kituo cha kazi. Mchakato wa ajira unazingatia misingi ya haki, usawa, na uwazi, kwa kuzingatia sifa stahiki zilizoainishwa katika tangazo la kazi husika na muundo wa utumishi wa idara inayohusika.

MAJINA ya Walioitwa Kwenye Usaili UTUMISHI

Tags:

About the Author ()

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

WhatsApp Channel Join Now!